logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mtuombee tafadhali! Mkewe Wafula Chebukati awasihi Wakenya

Mary Chebukati alifunguka jinsi kazi ya mumewe imemuweka mbali na familia yake.

image
na

Habari17 July 2022 - 13:16

Muhtasari


•"Saa zingine tunamwona kwa tv zaidi kuliko tunavyomwona nyumbani sababu ya hii kazi," Mary  alisema.

•Mary alibainisha kuwa wakati wa uchaguzi wa 2017 familia yao ilikuwa na wasiwasi mkubwa.

Mary Chebukati, mke wa mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Wafula Chebukati.

Huku zikiwa zimesalia siku 22 kufanyika kwa uchaguzi mkuu, Mke wa mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka Wafula Chebukati amewataka wakenya kumuombea.

"Naomba tu mtuombee, mtuombee kama familia wakati huu wenye tunaingia uchaguzi huu, mimi naomba mtuombee sababu mimi najua mzee kitu kimoja anataka kufuata sheria."

Akiongea wakati wa ibada ya mazishi siku ya Jumamosi, Mary alifunguka jinsi kazi ya mumewe imemuweka mbali na familia yake.

"Saa zingine tunamwona kwa tv zaidi kuliko tunavyomwona nyumbani sababu ya hii kazi," alisema.

Alibainisha kuwa wakati wa uchaguzi uliopita familia yao ilikuwa na wasiwasi mkubwa lakini mwaka huu wana nguvu zaidi.

"Wakati wa ule uchaguzi mwingine watoto walikuwa na huzuni sana lakini sasa wako na nguvu na hata yeye mwenyewe ako na nguvu na kila siku tunamuombea tukisema Mungu ampatie hekima, Mungu muoshe na damu ya Yesu ili atumikie nchi hii."

Mnamo Januari 18, 2017 Rais Uhuru Kenyatta alimteua Chebukati kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi akichukua hatamu kutoka kwa Issack Hassan.

 Akiwa na timu ya makamishna sita, Chebukati alisimamia uchaguzi Mkuu wa 2017 ambao ulikuwa na marudio ya uchaguzi wa urais mwezi Oktoba ambapo Rais Uhuru Kenyatta na William Ruto walitangazwa washindi.

Kwa uchaguzi wa mwaka huu, Chebukati amekuwa chini ya shinikizo la kuhakikisha uchaguzi huo unakuwa huru na wa haki, uliotawaliwa na dosari zozote

(Utafsiri: Samuel Maina)


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved