logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(Video) Nairobi! Jamaa avunja gari na kuiba shilingi milioni 1.4 mchana peupe

Mshukiwa alimfuata mhasiriwa kutoka benki moja mtaani Industrial Area hadi Kamukunji ambapo wizi huo ulifanyika.

image
na Radio Jambo

Burudani04 April 2022 - 08:29

Muhtasari


•Mshukiwa huyo anaripotiwa kumfuata mhasiriwa kutoka benki moja katika mtaa wa Industrial Area hadi mtaa wa Kamukunji ambapo wizi huo ulifanyika.

Polisi jijini Nairobi wanamsaka jamaa mmoja aliyenaswa na CCTV akivunja gari ndogo na kuiba kitita kikubwa cha pesa.

Katika kanda ya video ya CCTV inayoenezwa mitandaoni, mwanaume mwenye umri wa wastani aliyekuwa amevalia shati ya zambarau na suruali nyeusi alionekana akivunja gari ya bluu  na kuchukua kibahasha kinachoripotiwa kuwa na pesa taslimu Sh 1.4M.

Mshukiwa huyo anaripotiwa kumfuata mhasiriwa kutoka benki moja katika mtaa wa Industrial Area hadi mtaa wa Kamukunji ambapo wizi huo ulifanyika.

Kamera za CCTV  zilimnasa mshukiwa akifanya majaribio kadhaa ya kuvunja gari hilo na hatimaye akafaulu. Video hiyo inaonyesha mshukiwa akitafuta mahali pesa zimewekwa na hatimaye anaonekana akiondoka na kijibahasha kilichojaa pesa.

Tazama hapa:-


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved