logo

NOW ON AIR

Listen in Live

[Picha] Hafla ya mazishi ya hayati Mwai Kibaki yaendelea

Jeneza linalosheheni mwili wa hayati lilikuwa limefungwa kwa bendera ya Kenya

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 April 2022 - 08:18

Muhtasari


•Msafara wa mazishi ya Rais Mwai Kibaki umewasili katika uwanja wa Nyayo mwendo wa saa nne unusu asubuhi.

•Rais Uhuru Kenyatta  aliwasili katika uwanja wa Nyayo dakika chache kabla ya ibada ya mazishi ya Mwai Kibaki kung'oa nanga.

Marehemu Rais Mwai Kibaki akiwasili katika Uwanja wa Nyayo Aprili 29, 2022 kwa Ibada ya Mazishi ya Serikali.

Msafara wa mazishi ya hayati  Mwai Kibaki umewasili katika uwanja wa Nyayo mwendo wa saa nne unusu asubuhi.

Jeneza linalosheheni mwili wa hayati lilikuwa limefungwa kwa bendera ya Kenya.Kikosi cha wanajeshi wa KDF kilikuwa kimezidikisha jeneza hilo.

Mwili wa Kibaki wawasili katika uwanja wa Jomo Kenyatta
Mwili wa hayati Mwai Kibaki wawasili katika uwanja wa Nyayo
Gwaride la kijeshi katika uwanja wa Nyayo mnamo Aprili 29,2022

Rais Uhuru Kenyatta  aliwasili katika uwanja wa Nyayo dakika chache kabla ya ibada ya mazishi ya Mwai Kibaki kung'oa nanga.

Rais alipokelewa na naibu wake William Ruto.

Rais Uhuru Kenyatta katika hafla ya mazishi ya hayati Mwai Kibaki
Rais Uhuru Kenyatta apokewa na naibu wake William Ruto

Zaidi ya viongozi 10 wa mataifa mbalimbali ni miongoni mwa wageni maalum ambao wamehudhuria hafla hiyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved