logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(Picha) Maduka yafungwa jijini Nairobi wakenya wanaposibiri matokeo ya urais

Hali ya wasiwasi imetanda kote nchini huku maduka mengi tayari yakiwa yamefungwa katika  jiji kuu la Nairobi.

image
na Radio Jambo

Makala15 August 2022 - 12:41

Muhtasari


• Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alisema matokeo hayo yangetangazwa mwendo wa saa tisa alasiri.

•Hali ya wasiwasi imetanda kote nchini huku maduka mengi tayari yakiwa yamefungwa katika  jiji kuu la Nairobi.

Maduka kando ya mitaa ya Tom Mboga yamefungwa watu wameondoka.

Wakenya kote nchini wamesubiri kwa hamu na ghamu matangazo ya matokeo ya urais kutangazwa na tume ya uchaguzi na mipaka (IEBC).

Kupitia barua ya mwaliko kwa vyombo vya habari Jumatano asubuhi , Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alisema matokeo hayo yangetangazwa mwendo wa saa tisa alasiri.

Hata hicho kumekuwa na kuchelewa kwa matangazo ya matokeo hayo kufuatia sababu zisizothibitishwa.

Huku Wakenya wakisubiri kujua hatima ya uchaguzi uliofanyika Jumanne wiki jana, hali ya wasiwasi imetanda kote nchini huku maduka mengi tayari yakiwa yamefungwa katika  jiji kuu la Nairobi.

Tazama hali ilivyo Nairobi hapa:-

Maduka kando ya mitaa ya Tom Mboga yamefungwa watu wameondoka
Mtaa wa Taifa ni tupu watu wameondoka.

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved