logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(Picha) Wafuasi wa Azimio wajumuika nje ya Milimani kushuhudia uwasilishaji wa rufaa

Mawakili wa Raila tayari wamewasilisha rufaa kwa njia ya kielekroniki

image
na SAMUEL MAINA

Habari22 August 2022 - 09:00

Muhtasari


  • •Mawakili wa Raila wanatarajiwa kuwasilisha nakala ya rufaa katika mahakama ya Milimani kabla ya saa nane alasiri.
Wafuasi wa Azimio la Umoja wajumuika nje ya mahakama ya Milimani wakisubiri kuwasilishwa kwa rufaa la kupinga kuchaguliwa kwa William Ruto kama rais.

Mawakili wa mgombea urais wa Azimio Raila Odinga tayari wamewasilisha nakala ya kielektroniki ya rufaa ya kupinga ushindi wa Rais Mteule William Ruto.

Timu hiyo ya wanasheria hata hivyo wanatarajiwa kuwasilisha nakala ya rufaa katika mahakama ya Milimani kabla ya saa nane alasiri.

Baadhi ya wanasiasa wa Azimio tayari wamewasili katika mahakama hiyo kwa ajili ya kushuhudia kuwasilishwa kwa rufaa.

Umati wa wafuasi wa muungano huo pia walijitokeza nje ya mahakama ya Milimani Jumatatu asubuhi kumuunga mkono mgombea urais wao.

Baadhi ya wafuasi hao walionekana wakiwa wamebeba mabango ya kudai haki kutendeka. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved