logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi aenda mafichoni baada ya kumuua mwenzake kwa kumpiga risasi Nanyuki

Mshukiwa huyo ambaye ametambulishwa kama Titus Keen anadaiwa kutoroka na bunduki aina ya AK-47 iliyojaa risasi baada ya kutekeleza mauaji hayo.

image
na Radio Jambo

Habari19 August 2021 - 05:57

Muhtasari


•Polisi huyo anaripotiwa kumpiga risasi polisi mwenzake aliyetambulishwa kama Leonard Ojwang siku ya Jumatano katika kituo cha polisi cha Doldol.

Crime scene

Polisi wanamsaka afisa mmoja kutoka kituo kimoja cha polisi katika kaunti ya Laikipia anayedaiwa kumpiga risasi mwenzake na kumuua papo hapo.

Polisi huyo anaripotiwa kumpiga risasi polisi mwenzake aliyetambulishwa kama Leonard Ojwang siku ya Jumatano katika kituo cha polisi cha Doldol.

Mshukiwa huyo ambaye ametambulishwa kama Titus Keen anadaiwa kutoroka na bunduki aina ya AK-47 iliyojaa risasi baada ya kutekeleza mauaji hayo.

Bado haijabainika kilichoibua mzozo kati ya wawili hao uliopelekea maafa hayo huku uchunguzi zaidi ukiendelea kufanyika.

Tukio la polisi kuua mwenzake kwa kumpiga risasi  sio jambo geni nchini na hili ni tukio moja  tu la hivi karibuni kuripotiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved