logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa achoma sehemu za siri za mkewe na chai moto baada ya kumpata akisoma ujumbe aliotumiwa na mwanadada kwa simu yake

Sharon Chepkorir, 25, amesema kuwa mumewe Alfred Kigen, 32,  aliingia na kumpata akiandika nambari ya aliyekuwa ametuma ujumbe huo uliosoma "Mambo" na hapo ndipo akaendea chai iliyokuwa inaiva jikoni na kuimwaga kwenye sehemu zake za siri.

image
na Radio Jambo

Habari29 August 2021 - 12:54

Muhtasari


•Sharon Chepkorir, 25, amesema kuwa mumewe Alfred Kigen, 32,  aliingia na kumpata akiandika nambari ya aliyekuwa ametuma ujumbe huo uliosoma "Mambo" na hapo ndipo akaendea chai iliyokuwa inaiva jikoni na kuimwaga kwenye sehemu zake za siri.

crime scene

Jamaa mmoja kutoka kijiji cha Kapsir katika kaunti ya Bomet anaripotiwa kuchoma sehemu za siri za mkewe kwa chai moto baada ya kumpata akisoma ujumbe wa simu ambao ulikuwa umetumwa na mwanadada mwingine kwa simu yake. 

Sharon Chepkorir, 25, amesema kuwa mumewe Alfred Kigen, 32,  aliingia na kumpata akiandika nambari ya aliyekuwa ametuma ujumbe huo uliosoma "Mambo" na hapo ndipo akaendea chai iliyokuwa inaiva jikoni na kuimwaga kwenye sehemu zake za siri.

"Nilikuwa nimeshika simu ya mzee nikapata ujumbe wa mtu mwingine nikachukua namba. Mzee wangu akanipata nikiwa natoa namba kwa simu yake. Alipoona namba ambayo nilikuwa nimeandika akaenda jikoni akatoa chai kwa moto alafu akanichoma nayo kwenye sehemu za siri. Saa hii hata siwezi kuenda msalani" Chepkorir alieleza wanahabari siku ya Jumapili akiwa nyumbani kwa wazazi wake ambako anaendelea kuponya majeraha.

Mama huyo wa watoto watatu ambaye alionekana kulemewa kutembea vizuri aliugua majeraha mabaya sio tu kwenye sehemu za siri mbali pia kwenye mapaja yake.

Mwanamke aliyekuwa amemtumia Kigen ujumbe ulioibua mzozo anadaiwa kuwa mpango wake wa kando.

Kulingana na familia ya Sharon, sio mara ya kwanza wanandoa hao wawili wamekuwa wakizozana na mara kwa mara ugomvi umeibuka kati yao. Wametoa ombi kwa serikali kuchukua hatua kali dhidi ya mshukiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved