logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DP Ruto akana kumiliki mali zilizoorodheshwa na waziri Matiang’i mbele ya wabunge

Akijitokeza mbele ya Kamati ya Bunge ya Utawala na Usalama wa Kitaifa Jumanne

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 September 2021 - 14:42

Muhtasari


  • Naibu Rais William Ruto amekataa kumiliki mali zingine zilizoorodheshwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Fred Matiang’i

Naibu Rais William Ruto amekataa kumiliki mali zingine zilizoorodheshwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Fred Matiang’i.

Akijitokeza mbele ya Kamati ya Bunge ya Utawala na Usalama wa Kitaifa Jumanne, CS alisema DP ana maafisa 51 walioshikilia mali zake.

Gesi ya Kitengela ina maafisa sita, Weston Hoteli ina maafisa wanne wakati Shamba la Murumbi lina maafisa sita.

Ranch ya ADC Laikipia Mutara ina maafisa sita, Hoteli ya Dolphine huko Mombasa ina sita, Mata Farm ina sita na makao ya kibinafsi ya DP huko Elgon View Eldoret yana wanne.

Walakini, masaa kadhaa baadaye, katibu wa mawasiliano wa Ruto David Mugonyi alitupilia mbali ripoti hiyo iliyowasilishwa.

"Kuelewa uzembe wa Matiangi, mali nyingi zilizopewa Naibu Rais katika taarifa yake kwa Bunge kwa kweli sio zake," Mugonyi alisema kupitia taarifa.

Kulinga na stakabdhi zilizowasilishwa katika kamati ya bunge ya ulinzi na waziri wa Usalama Fred Matiangi siku ya Jumatano naibu rais analindwa na jumla ya maafisa 257 wa polisi.

"Hatujadunisha usalama wa naibu huyo. Mabadiliko mapya walifanywa na Inspekta mkuu wa polisi. Utaratibu huo ulikuwa sawa ," Matiang'i alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved