logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume mwenye kifafa afariki baada ya kuanguka juu ya makaa moto aliyokuwa anachoma Nakuru

Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 42 na ambaye ni mwathiriwa wa kifafa alizirai na kuangukia makaa moto ambayo alikuwa anachoma katika kijiji kilicho kwenye mpaka wa kaunti ya  Nakuru na Narok.

image
na Radio Jambo

Habari08 September 2021 - 07:33

Muhtasari


•Alizirai na kuangukia makaa moto ambayo alikuwa anachoma katika kijiji kilicho kwenye mpaka wa kaunti ya  Nakuru na Narok.

crime scene

Mwanaume mmoja  kutoka eneo ya Eburru, kaunti ya Nakuru alifariki dunia baada ya kuanguka juu ya makaa ambayo alikuwa anatayarisha.

Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 42 na ambaye ni mwathiriwa wa kifafa alizirai na kuangukia makaa moto ambayo alikuwa anachoma katika kijiji kilicho kwenye mpaka wa kaunti ya  Nakuru na Narok.

Alipokuwa anathibitisha tukio hilo, OCPD wa eneo hilo alisema  kuwa uchunguzi zaidi umeanzishwa kubaini kilichotokea.

"Mwanaume huyo alikuwa na kifafa na alikuwa anachoma makaa wakati alinguka kwenye moto na kuchomeka vibaya hadi akaaga" bosi wa polisi alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved