logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bangi na lita 107 za pombe haramu zapatikana Mlolongo

Hata hivyo hakuna yeyote aliyekamatwa kwani wenye shehena waliweza kutoroka baada ya kupata taarifa kuwa kulikuwa na msako ulikuwa unaendelea.

image
na Radio Jambo

Burudani09 September 2021 - 03:05

Muhtasari


•Shehena hiyo ambayo ilipatikana wakati wa msako uliofanywa katika eneo la Kapa, Syokimau ilikuwa pamoja na lita 77 za chang'aa, lita 30 za kangara, kilo 20 na misokoto 78 ya bangi.

•Hata hivyo hakuna yeyote aliyekamatwa kwani wenye shehena waliweza kutoroka baada ya kupata taarifa kuwa kulikuwa na msako ulikuwa unaendelea.

Madawa ya kulevya ambayo yalipatikana Mlolongo

Zaidi ya lita 100 za pombe haramu na bangi zilipatikana maeneo ya Mlolongo kaunti ya Machakos siku ya Jumatano.

Shehena hiyo ambayo ilipatikana wakati wa msako uliofanywa katika eneo la Kapa, Syokimau ilikuwa pamoja na lita 77 za chang'aa, lita 30 za kangara, kilo 20 na misokoto 78 ya bangi.

Operesheni hiyo ilifanywa na naibu kamishna wa eneo la Mlolongo Dennis Ongaga, kamanda wa polisi katika kituo cha Syokimau Hamisi Chivasi, chifu wa Mlolongo Peter Ndunda, naibu chifu wa Syokimau David Kilonzo,naibu chifu wa Mlolongo Florence Kiio pamoja na maafisa wengine.

Hata hivyo hakuna yeyote aliyekamatwa kwani wenye shehena waliweza kutoroka baada ya kupata taarifa kuwa kulikuwa na msako ulikuwa unaendelea.

Naibu Kamishna Ongaga alisema kuwa shehena hiyo itaharibiwa iwapo hawataweza kukamata washukiwa.

Ongaga alisema kuwa ni ngumu kuweza kukamata yeyote katika eneo la Kapa kwani kuna pingamizi kubwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved