logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa wawili watiwa mbaroni kwa kushirikiana kubaka mwanamke mwenye ulemavu wa akili Lamu

Ngumi alipigwa na butwaa kubwa aliporejea na kupata Murimi akijitosheleza kimapenzi na mwanadada yule mwenye umri wa wastani huku Kokane akiwa ashatoroka baada ya kumaliza zamu yake ya kukata kiu cha mapenzi na mwanamke yule.

image
na Radio Jambo

Habari15 September 2021 - 02:18

Muhtasari


•Wawili hao walikuwa wameandamana na mzee wa nyumba kumi aliyetambulishwa kama Samuel Ngumi walipopata mwanamke mwenye ulemavu wa kiakili akitengeneza chai katika maeneo yasiyo salama.

•Ngumi alipigwa na butwaa kubwa aliporejea na kupata Murimi akijitosheleza kimapenzi na mwanadada yule mwenye umri wa wastani huku Kokane akiwa ashatoroka baada ya kumaliza zamu yake ya kukata kiu cha mapenzi na mwanamke yule.

crime scene

Polisi katika kaunti ya Lamu wanazuilia jamaa wawili ambao wanadaiwa kushirikiana kubaka mwanamke mwenye ulemavu wa kiakili.

Shadrack Murimi 45 na Hiribae Kokane 43,  wanaripotiwa kubaka mwanamke huyo mida ya saa mbili usiku wa Jumatatu walipokuwa wanashika doria katika eneo la  Sina Mbio.

Kulingana na DCI, wawili hao walikuwa wameandamana na mzee wa nyumba kumi aliyetambulishwa kama Samuel Ngumi walipopata mwanamke mwenye ulemavu wa kiakili akitengeneza chai katika maeneo yasiyo salama.

Kufuatia hayo, mzee Ngumi alienda kutafutia mwanamke yule usaidizi na kuacha kama ameagiza washukiwa wabaki wakimlinda.

Ngumi alipigwa na butwaa kubwa aliporejea na kupata Murimi akijitosheleza kimapenzi na mwanadada yule mwenye umri wa wastani huku Kokane akiwa ashatoroka baada ya kumaliza zamu yake ya kukata kiu cha mapenzi na mwanamke yule.

Mzee Ngumi alisaidiana na wakazi kunusuru mwanamke huyo kisha kufahamisha polisi ambao waliwakamata jamaa wale na kuwatia korokoroni.

Mhasiriwa alipelekwa  kufanyiwa vipimo vya kidaktari katika zahanati ya Hindi Magogoni. Murimi na Kokane watafikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa ubakaji pindi wapelelezi watakamilisha uchunguzi wa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved