logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hofu Nyeri baada ya mwili wa msichana aliyekuwa ametoweka kupatikana umetupwa ndani ya mto

Margret Waithera ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya upili ya Ngamwa aliripotiwa kutoweka  takriban wiki tatu zilizopita.

image
na Radio Jambo

Habari22 September 2021 - 03:40

Muhtasari


•Margret Waithera ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya upili ya Ngamwa aliripotiwa kutoweka  takriban wiki tatu zilizopita.

•Mwili wa msichana huyo uliashiria dalili kuwa alikuwa amebakwa kabla ya kuuawa na watu wasiojulikana.

Hali ya majonzi imetanda katika kijiji cha Mutonga eneo la Mukurweini, Nyeri baada ya mwili wa msichana wa miaka 13 kupatikana ukiwa umetupwa ndani ya mto Rwarai.

Margret Waithera ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya upili ya Ngamwa aliripotiwa kutoweka  takriban wiki tatu zilizopita.

Familia ya marehemu imekuwa ikimtafuta tangu atoweke bila mafanikio  na ndoto yao ya kupatanishwa tena na binti wao ilikatizwa baada yake kupatikana akiwa maiti.

Inaripotiwa kuwa mwili wa marehemu ulipatikana na wavuvi ukiwa umefungwa kwa gunia. 

Mwili wa msichana huyo uliashiria dalili kuwa alikuwa amebakwa kabla ya kuuawa na watu wasiojulikana.

Upelelezi zaidi kuhusiana na kisa hicho umeng'oa nanga huku familia ya marehemu ikianza mipango ya kumzika mpendwa wao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved