logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge wa Mvita awapoteza wafanyakazi 4 katika ajali mbaya ya barabarani

Kulingana na ODM hao wanne walikuwa wafanyikazi wa Mbunge huyo

image
na Radio Jambo

Habari14 November 2021 - 08:47

Muhtasari


  • Chama cha ODM kilithibitisha kisa hicho katika ujumbe wa Twitter kikisema wanne hao waliaga dunia Jumamosi jioni

Mbunge wa Mvita Abdulswamad Nassir amepoteza wanachama wanne wa timu yake kwenye ajali mbaya ya barabarani.

Chama cha ODM kilithibitisha kisa hicho katika ujumbe wa Twitter kikisema wanne hao waliaga dunia Jumamosi jioni.

Kulingana na ODM hao wanne walikuwa wafanyikazi wa Mbunge huyo. Kulingana na ripoti ya polisi, walifariki baada ya gari walilokuwa wakisafiria kubingiria baada ya tairi kupasuka.

“Tunasikitika kupata taarifa ya kifo cha wanachama 4 wa timu ya Mh.Nassir ambao ni Ali Omar Naaman, Bi Carol Wayua Mueni, Athman Mohammed Omar na Elysian Musyoka kupitia ajali mbaya ya barabarani jioni ya leo. Tunaziombea familia za marehemu. wakati huu mgumu," taarifa ya ODM ilisoma.

Kutoka kwetu wanajambo Mungu azidi kulaza roho zao mahal pema peponi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved