logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume mmoja kujifunga kwa minyororo kwenye lango la ofisi ya DP Ruto akidai anataka kazi

Kwa hivyo alisema kuwa ataondoka tu baada ya DP Ruto kushughulikia lalama zake binafsi.

image
na Radio Jambo

Habari11 January 2022 - 13:53

Muhtasari


  • Msemaji wa Ruto Emmanuel Talam alisema suala hilo limeshughulikiwa
  • Kwa hivyo alisema kuwa ataondoka tu baada ya DP Ruto kushughulikia lalama zake binafsi

DP William Ruto Jumanne alilazimika kuingilia kati baada ya mwanamume mmoja kujifunga kwa minyororo kwenye lango la ofisi yake ya Harambee Annex kwa kukosa kazi.

Msemaji wa Ruto Emmanuel Talam alisema suala hilo limeshughulikiwa.

"DP amepanga yaliyotolewa na kuitaka ofisi yake kushughulikia kesi ya kijana huyo," Talam alisema.

Lawrence Oprong awali alichukuliwa na maafisa wa polisi ambao walimpeleka hadi kituo cha polisi cha Central.

Kulingana na ripoti nyingi, mwanamume huyo aliyetambulika kama Lawrence Amuke Oprong alifunga mnyororo kiunoni kwenye lango la jengo hilo kwa kutumia cheni na kufuli akitaja kuwa Naibu Rais alikuwa amemuahidi kazi lakini akafeli. kutimiza ahadi yake.

Kwa hivyo alisema kuwa ataondoka tu baada ya DP Ruto kushughulikia lalama zake binafsi.

Oprong anayedai kuwa mtoto wa aliyekuwa Mbunge wa Busia Kaskazini Fredrick Oduya Oprong alisema alikuwa ameahidiwa kazi miaka minne iliyopita.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved