logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fahamu jinsi unavyoweza kusajili Simcard yako ya Safaricom mtandaoni bila kutembelea kituo

Kampuni ya Safaricom imezindua njia ya kutekeleza shughuli hiyo mtandaoni.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 April 2022 - 10:45

Muhtasari


•Siku ya Ijumaa, CA iliongeza muda wa makataa wa usajili wa simu kwa miezi sita hadi Oktoba 15, 2022.

Smart phone

Huku  Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (CA) ikiwa imetoa amri kwa watumizi wa huduma za simu kusajili SimCards zao, Kampuni ya Safaricom imezindua njia ya kutekeleza shughuli hiyo mtandaoni.

Hii ni baada ya Wakenya kulalamika kwenye mitandao ya kijamii wakiomba kampuni hiyo kufuata nyayo za Telkom ambao tayari walikuwa wameanzisha usajili wa Sim Card mtandaoni.

Siku za hivi majuzi foleni ndefu zimeshuhudiwa katika vituo  mbalimbali vya usajili wa laini kote nchini huku Wakenya wakiwa mbioni kuepuka kufungiwa.

Siku ya Ijumaa, CA iliongeza muda wa makataa wa usajili wa simu kwa miezi sita hadi Oktoba 15, 2022.

Watumizi wa simu ambao hawatakuwa wamesajili laini zao kufikia Oktoba 15 wanahatarisha kufungiwa laini zao.

Ili kusajili laini yako mtandaoni, fuata maelezo yaliyo kwenye link hii>>>


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved