logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbwa wawaua mama na mwanawe Ugenya

Mbwa hao walifugwa katika boma moja eneo la Siranga.

image
na

Yanayojiri02 May 2022 - 09:54

Muhtasari


  • Akithibitisha kisa hicho, naibu OCPD wa Ugenya James Ngao alisema kuwa Caren Akinyi Aluoch mwenye umri wa miaka 28 aliuawa pamoja na mtoto wake wa kiume wa mwaka mmoja
Mbwa waliofungiwa kwa ajili ya kuchinjwa huko Korea

Mama na mwana wameuawa na mbwa katika eneo la Simur, Kaunti Ndogo ya Ugenya.

Mbwa hao walifugwa katika boma moja eneo la Siranga.

Kulingana na meneja wa nyumba hiyo, mbwa hao wakali walikuwa wametoroka kutoka kwenye banda lao Jumapili usiku na majaribio ya kuwatafuta hayakufaulu.

Akithibitisha kisa hicho, naibu OCPD wa Ugenya James Ngao alisema kuwa Caren Akinyi Aluoch mwenye umri wa miaka 28 aliuawa pamoja na mtoto wake wa kiume wa mwaka mmoja.

"Msimamizi wa nyumba aliripoti kwamba mbwa walikuwa wametoka nje ya boma. Mwanamke huyo na mtoto wake walipatikana Jumatatu asubuhi wakiwa wamepasuliwa na mbwa hao wakatili,” Ngao alisema.

Wenyeji waliwapiga mbwa hadi kufa.

Miili ya bibi huyo na mwanawe imepelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha kaunti ndogo ya Ukwala.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved