logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru, Ruto wakutana katika kikao cha baraza la mawaziri Ikulu

Taarifa kutoka Ikulu ilisema masuala ya umuhimu ya kitaifa na kimataifa yatajadiliwa

image
na Radio Jambo

Burudani12 May 2022 - 11:22

Muhtasari


  • Haya yanajiri baada ya Naibu Rais Ruto kudai kuwa hakuhudhuria vikao vya baraza la mawaziri baada ya majukumu yake kudaiwa kukabidhiwa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i

Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto walikutana Alhamisi kwa mkutano wa Baraza la Mawaziri.

Wawili hao walikutana katika Ikulu ya Nairobi, ambapo mkuu wa nchi ndiye anaongoza mkutano huo kwa sasa.

Taarifa kutoka Ikulu ilisema masuala ya umuhimu ya kitaifa na kimataifa yatajadiliwa wakati wa mkutano huo.

"Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta leo yuko Ikulu, Nairobi, akiongoza kikao kamili cha Baraza la Mawaziri ambapo masuala kadhaa ya umuhimu wa kitaifa na kimataifa yatajadiliwa."

Haya yanajiri baada ya Naibu Rais Ruto kudai kuwa hakuhudhuria vikao vya baraza la mawaziri baada ya majukumu yake kudaiwa kukabidhiwa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i.

Ruto amekosekana katika mikutano ya awali ya Baraza la Mawaziri.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved