logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi wamsaka mshukiwa kwa mauaji ya mwanafunzi Kiambu, mwili kutupwa kando ya barabara

Mwili wake ulihamishwa hadi katika chumba cha kuhifadhia maiti cha City jijini Nairobi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 May 2022 - 08:06

Muhtasari


  • Mwili wake ulipatikana umetupwa kando ya barabara karibu na mtaa wa Mburiria mapema Jumamosi asubuhi

Maafisa wa upelelezi katika Kaunti ya Kiambu wanamsaka mwanamume aliyejulikana kama VDJ Flex ambaye anahusishwa na mauaji ya mwanafunzi wa chuo mwenye umri wa miaka 19.

Purity Wangeci Kiringa anasemekana kuondoka chuoni siku ya Ijumaa ili kumtembelea mpenziwe eneo la Kirigiti, Kaunti ya Kiambu.

Mwili wake ulipatikana umetupwa kando ya barabara karibu na mtaa wa Mburiria mapema Jumamosi asubuhi, ukiwa na majeraha ya kuchomwa kisu na kunyongwa.

Makachero kutoka Idara ya Upelelezi ya Makosa ya Jinai (DCI) walibaini kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 19 aliuawa sehemu nyingine na mwili wake kutupwa katika eneo la tukio, ambapo hati zake za utambulisho, matandiko yenye damu na nguo pia zilipatikana.

Kulingana na marafiki zake waliozungumza na wapelelezi, wenzi hao walikuwa na ugomvi hivi majuzi "baada ya kugundua kwamba alikuwa jambazi na kumkabili na ukweli."

Mwili wake ulihamishwa hadi katika chumba cha kuhifadhia maiti cha City jijini Nairobi kusubiri uchunguzi wa maiti yake, huku wapelelezi wakimfuatilia mshukiwa.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved