logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi wanamsaka mwanamume anayeshukiwa kumuua bintiye Kajiado

Kalovya alisema mshukiwa alikuwa akiishi na familia yake katika Kaunti ya Kajiado

image
na Radio Jambo

Habari12 June 2022 - 11:12

Muhtasari


  • Polisi wanamsaka mwanamume anayeshukiwa kumuua bintiye Kajiado

Polisi wanamsaka mwanamume ambaye yuko mafichoni baada ya kudaiwa kumuua bintiye wa umri wa miaka 11 na kumjeruhi mwanawe siku ya Jumamosi.

Kulingana na msimamizi wa kijiji Willy Kalovya, mwanamume huyo wa umri wa makamo alitoroka baada ya kisa hicho katika kijiji cha Kilungu B katika Kaunti Ndogo ya Kibwezi, Kaunti ya Makueni mwendo wa saa sita usiku.

Kalovya alisema mshukiwa alikuwa akiishi na familia yake katika Kaunti ya Kajiado na alikuwa amefika Jumamosi nyumbani kwake kijijini na watoto wake wawili. Aliongeza kuwa mshukiwa huyo amekuwa na tofauti za ndoa na mkewe, jambo ambalo lilisababisha hali hiyo mbaya.

Mvulana aliyejeruhiwa tangu wakati huo amekimbizwa katika hospitali ya Kaunti Ndogo ya Kibwezi kwa matibabu.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved