logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Hakuna likizo kwa maafisa wa polisi!" - Hillary Mutyambai

“Kutokana na uchaguzi mkuu ujao, hakuna afisa anayepaswa kupewa likizo kuanzia Julai 1, 2022, isipokuwa kwa misingi ya matibabu" - IG

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 July 2022 - 06:02

Muhtasari


• "Maafisa wote waliokuwa likizoni wataitwa na kuwa kazini ifikapo tarehe 4 Julai 2022,” - IG

Inspekta jenerali wa polisi Hillary Mutyambai amesitisha mipango yote ya kuwapa maafisa wa polisi likizo hadi baada ya uchaguzi mkuu wa Agosti 9.

Kulingana na taarifa iliyopakiwa kwenye ukurasa wa Facebook wa tume ya huduma kwa polisi NPS kutoka kwa gazeti moja la humu nchini, inaarifiwa kwamba naibu inspekta jenerali wa polisi, Edward Mbugua alituma kumbukumbu kwa makamanda wa mikoa na kuwataka waarifu maafisa wote wa polisi walioko kwenye likizo kurejea kazini mara moja.

Kumbukumbu hiyo iliwapa maafisa walioko kwenye likizo hadi Julai 4 wawe wamerejelea majukumu yao kama kawaida.

“Kutokana na uchaguzi mkuu ujao, hakuna afisa anayepaswa kupewa likizo kuanzia Julai 1, 2022, isipokuwa kwa misingi ya matibabu na mapendekezo ya madaktari. Maafisa wote waliokuwa likizoni wataitwa na kuwa kazini ifikapo tarehe 4 Julai 2022,” gazeti hilo lilinukuu kumbukumbu hiyo.

Maafisa wa polisi wamekuwa wakipewa mafunzo jinsi ya kusaidia tume ya uchaguzi na mipaka IEBC kuendesha uchaguzi kwa amani bila vurugu zozote.

Juzi Waziri wa usalama wa ndani Dkt. Fred Matiang’I aliwataka walimu na polisi kujiepusha na siasa za marengo taifa linapojiandaa kuelekeqa uchaguzi mkuu wa Agosti 9 na kuwataka kukoma kushiriki katika vitendo vya kisiasa kwa sababu wao vi watoa huduma kwa umma na hivyo hawafai kuonesha wazi marengo wanayoipendelea.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved