logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DP Ruto amuomboleza mwigizaji wa filamu Nairobi Half Life Olwenya Maina

Wakati huo huo, uchunguzi kuhusu kifo cha ghafla cha Olwenya umeanza.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 July 2022 - 11:43

Muhtasari


  • Katika ujumbe wake wa rambirambi, DP alimkumbuka Olwenya kama mwigizaji mahiri ambaye ametoka jukwaani hivi karibuni

Naibu Rais William Ruto ameomboleza mwigizaji Maina Olwenya aliyeaga dunia Jumatatu usiku baada ya kuzirai.

Katika ujumbe wake wa rambirambi, DP alimkumbuka Olwenya kama mwigizaji mahiri ambaye ametoka jukwaani hivi karibuni.

"Ninaomboleza pamoja na familia, marafiki na wafanyakazi wenzangu. Tumepoteza talanta ya kweli, mbunifu aliyejitolea na mtu mzuri. Kama vile talanta zote kuu, Maina ataendelea na kazi yake. Safiri Salama," Ruto alisema.

Olwenya, ambaye aliigiza Oti katika filamu ya Nairobi Half Life 2012, alitangazwa kuwa amefariki katika hospitali ya Nairobi ambapo alikimbizwa baada ya kuzirai.

Chanzo cha kifo bado hakijajulikana lakini familia hiyo, ambayo imetaka kuwepo kwa utulivu na faragha wakati huu, itatoa taarifa zaidi ikiwa tayari.

Wakati huo huo, uchunguzi kuhusu kifo cha ghafla cha Olwenya umeanza.

Olwenya pia alifanya kazi kama msanii wa sauti katika matangazo mbalimbali.

PIa amewahi fanya matangazo kwenye Radiojambo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved