logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume apatikana amekufa katika makazi yake Machakos

Msimamizi huyo alisema marehemu alikuwa mwendawazimu kabla ya kuchomwa moto.

image
na

Yanayojiri07 July 2022 - 12:22

Muhtasari


  • Mwanamume apatikana amekufa katika makazi yake Machakos
  • Maafisa wa DCI kutoka kituo hicho wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo

Mwanamume mmoja amepatikana akiwa amefariki katika nyumba iliyotelekezwa inayoshukiwa kuwa makazi yake huko Athi River, Kaunti ya Machakos.

Chifu msaidizi wa Athi River Martin Ngomo alisema mwili huo uligunduliwa katika nyumba hiyo iliyotelekezwa na wapita njia mwendo wa saa 11.00 asubuhi Alhamisi.

Nyumba ambayo mwili huo ulipatikana ukiwa katika shamba la Embakasi haina paa wala milango.

"Tulipokea simu mwendo wa saa 10.00 asubuhi kwamba kulikuwa na kijana aliyeungua. Aliteketea kiasi cha kutotambulika katika eneo la mji wa Athi River ndani ya kaunti ndogo ya Athi River," Ngomo aliambia Radiojambo katika eneo la tukio Alhamisi.

Msimamizi huyo alisema marehemu alikuwa mwendawazimu kabla ya kuchomwa moto.

Ngomo alisema mtu huyo anafahamika sana na wakazi kwa jina la utani, profesa.

Aliwaambia wakazi kuwa waangalifu hasa wanapotumia moto.

Inashukiwa kuwa godoro alilokuwa amelalia iliwaka  moto na kusababisha kifo chake.

Polisi kutoka kituo cha polisi cha Athi River waliuondoa mwili huo hadi katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Machakos Level 5.

Sababu ya moto haikujulikana mara moja.

Maafisa wa DCI kutoka kituo hicho wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved