logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kenya yatoa siku saba kwa Facebook kujielezea kuhusu udhibiti dhaifu wa maudhui

Facebook ilishindwa kugundua matangazo yenye maudhui ya uchochezi yaliyochapishwa kwa Kiingereza na Kiswahili.

image
na Radio Jambo

Habari30 July 2022 - 04:33

Muhtasari


•Tume ya uwiano na utangamano wa kitaifa nchini imetishia kusimamisha matumizi ya mtandao wa Facebook kwa madai ya kukiuka sera za matamshi ya chuki.

•Global Witness na Foxglove, inasema kwamba Facebook ilishindwa kugundua matangazo yenye maudhui ya uchochezi yaliyochapishwa kwa Kiingereza na Kiswahili.

Tume ya uwiano na utangamano wa kitaifa nchini Kenya imetishia kusimamisha matumizi ya mtandao wa Facebook kwa madai ya kukiuka sera za matamshi ya chuki.

Tume hiyo ya Kitaifa inasema imeiandikia Meta ikitaka majibu kwa madai ya udhibiti dhaifu wa maudhui kwenye Facebook kabla ya uchaguzi wa mwezi ujao.

Kamishna wa Ttume Dkt. David Makori alikuwa akijibu matokeo ya ripoti ya Global Witness na Fox Glove ambayo ilionyesha kuwa Facebook imeshindwa kudhibiti maudhui kwenye jukwaa lake kutokana na udhibiti dhaifu.

"Ikiwa Facebook haitatii mahitaji ambayo tumeweka ndani ya siku saba, tutapendekeza wasitishe shughuli zao. Hatutaruhusu Facebook kuhatarisha usalama wetu wa taifa”, Makori alisema.

Tume haina mamlaka ya kusimamisha Facebook lakini inaweza tu kupendekeza kwa mamlaka ikiwa kampuni itashindwa kufuata miongozo kama ilivyoainishwa katika sheria.

Ripoti ya mashirika ya utetezi ya Global Witness na Foxglove, inasema kwamba kampuni hiyo kubwa ya mitandao ya kijamii ilishindwa kugundua matangazo yenye maudhui ya uchochezi kwenye jukwaa lake yaliyochapishwa kwa Kiingereza na Kiswahili.

Wakati wa uchunguzi, watafiti waliwasilisha matangazo 20 yenye lugha ya chuki kutoka katika uchaguzi wa 2007 yaiyochapishwa katika lugha zote mbili. Ripoti hiyo inasema matangazo yote yaliyowasilishwa yaliidhinishwa isipokuwa moja la Kiingereza kwa kutofuata miongozo yake kuhusu matamshi ya chuki.

Global witness inasema matangazo hayajawahi kuchapishwa kwenye Facebook lakini walishangazwa na namna yalivyopita bila kutambuliwa.

Facebook haijajibu matokeo ya ripoti hii.

Mnamo Julai, kampuni ya teknolojia iliripoti kuwaondoa watumiaji 37,000 kwa kuchochea matamshi ya chuki na 42,000 kwa kukiuka ghasia na sera zake za uchochezi wakati wa uchaguzi wa Agosti.

Kampuni hiyo pia ilisema kuwa imekataa matangazo 36,000 ya kisiasa kwa kutofuata sheria zake za uwazi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved