logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kalonzo ajiondoa kutoka kinyang’anyiro cha spika wa seneti muda mchache kabla ya uchaguzi

Muungano wa Azimio Jumatano uliafikia kumuunga mkono Kalonzo kuwa Spika wa seneti.

image
na Radio Jambo

Habari08 September 2022 - 09:57

Muhtasari


• Hatua hiyo ya Kalonzo ilitangazwa na katibu wa Seneti Jeremiah Nyegenye.

Muungano wa Azimio umepata pigo baada ya mgombea wa muungano huo kwa wadhifa wa spika wa seneti Kalonzo Musyoka kujiondoa kutoka kinyang’anyiro hicho.

Hatua hiyo ya Kalonzo ambaye pia ni kinara wa chama cha Wiper ilitangazwa na katibu wa Seneti Jeremiah Nyegenye.

Nyegenye alisema kwamba ofisi yake ilikuwa imepokea barua asubuhi siku ya Alhamisi kutoka kwa Kalonzo akiondoa azma yake.

Maseneta katika muungano wa Azimio siku ya Jumatano walikuwa wameafikia kwa kauli moja kumuunga mkono Kalonzo kwa wadhifa wa Spika wa seneti.

Aliyekuwa gavana wa Kilifi Amason Kingi ambaye anapendekezwa na muungano wa Kenya Kwanza alikuwa mpinzani mkuu wa Kalonzo.

Mapema Jumahili Kalonzo alikuwa amechukuwa stabadhi za kuania wadhifa wa spika katika bunge la kitaifa na Seneti lakini akabadili mawazo na kujiondoa kutoka kinyang’anyiro cha spika wa bunge la Kitaifa ili awanie nafasi ya spika wa seneti.

Bado haijabainika sababu kuu ya Kalonzo kujiondoa kutoka kinyang’anyiro cha spika wa seneti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved