logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kalonzo ahudhuria sherehe za Mashujaa Uhuru Gardens

Mnamo Septemba, kiongozi huyo wa Wiper alipuuzilia mbali madai kwamba aliwasiliana na Rais.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri20 October 2022 - 09:41

Muhtasari


  • Mnamo Septemba, kiongozi huyo wa Wiper alipuuzilia mbali madai kwamba aliwasiliana na Rais
  • Kalonzo alisema uvumi huo kwenye mitandao ya kijamii ni ubunifu wa watu wenye nia mbaya
  • Alisema atakutana na Ruto hadharani kwa wakati ufaao, lakini baada ya kushauriana na uongozi wa Wiper na Azimio

Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka alihudhuria sherehe za Mashujaa Day katika bustani ya Uhuru Gardens.

Huenda alikuwa kiongozi pekee wa Muungano wa Azimio la Umoja One aliyehudhuria sherehe za 59 za Mashujaa Day.

Kalonzo aliketi kwenye jukwaa la watu mashuhuri na hata alilakiwa na Rais William Ruto alipofika.

Mnamo Septemba, kiongozi huyo wa Wiper alipuuzilia mbali madai kwamba aliwasiliana na Rais.

Kalonzo alisema uvumi huo kwenye mitandao ya kijamii ni ubunifu wa watu wenye nia mbaya.

Alisema atakutana na Ruto hadharani kwa wakati ufaao, lakini baada ya kushauriana na uongozi wa Wiper na Azimio.

Wiki iliyopita, Kalonzo alimsihi Rais afikirie upya msimamo wake kuhusu kuondoa marufuku ya vyakula vya GMO nchini.

Kuwepo kwake kulikuja kwa mshangao, kutokana na msimamo wake wa awali kwamba Azimio hatajihusisha na serikali kwa njia nyingine yoyote isipokuwa kuidhibiti.

Aidha iliibua uvumi iwapo kinara wa chama cha muungano huo Raila Odinga, ambaye yuko nje ya nchi kwa safari ya siku 10 , alifahamu kuwa alikuwa akihudhuria hafla hiyo.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved