logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Tuwalinde watu wetu,'Millicent Omanga,Ngujiri wasema baada ya seneta Cherargei kusema ameibiwa

Kauli yake inajiri dakika chache tu baada ya Cherargei kufichua kwamba aliibiwa

image
na Radio Jambo

Habari15 November 2022 - 17:46

Muhtasari


  • Omanga sasa amesema kuwa ni wakati wa serikali kuchukua hatua madhubuti dhidi ya magenge ya wahalifu yanayoendesha fujo jijini
Seneta mteule Millicent Omanga

Millicent Omanga sasa ametangaza kwamba sasa ni wakati wa wahalifu wa Nairobi kukabiliana na polisi dakika chache baada ya Seneta wa Nandi Samson Kiprotich Arap Cherargei kufichua kwamba aliibiwa na wahalifu akiwa kwenye msongamano wa magari.

Omanga sasa amesema kuwa ni wakati wa serikali kuchukua hatua madhubuti dhidi ya magenge ya wahalifu yanayoendesha fujo jijini.

Kauli yake inajiri dakika chache tu baada ya Cherargei kufichua kwamba aliibiwa alipokuwa kwenye trafiki kwenye Barabara ya Valley.

Cherargei alikuwa amesimulia jinsi akiwa amekwama kwenye barabara ya bondeni yenye shughuli nyingi, jambazi jasiri aliondoa kioo chake huku akisema kuwa Nairobi imekuwa jiji la uhalifu na kimbilio la magenge.

Alitoa wito kwa serikali kushughulikia hali ya usalama mara moja kwa kupanga upya sekta ya usalama.

"Wiki moja iliyopita nilipoteza kioo cha upande wa kushoto cha gari langu nikiwa nimekwama kwenye msongamano wa magari  kando ya Valley Road kiliondolewa kwa nguvu na jambazi. Nairobi sasa ni jiji la uhalifu na kimbilio la magenge. Kudorora kwa usalama kote nchini lazima kushughulikiwe mara moja kwa kupanga upya sekta ya usalama,"Cherargei alisema.

Huku Millient Omanga akizungumzia hali ya usalama alisema kuwa;

"Wakati wa kuchukua hatua madhubuti dhidi ya magenge ya wahalifu yanayoendesha ghasia jijini."

Aliyekuwa mbunge wa Nyeri Ngunjiri Wambugu akiunga mkono maoni ya Omanga alisema kwamba ni jukumu la serikali kuliwalinda wananchi.

"Naamini  hon kindiki lazima aweke juhudi zaidi za kushughulikia masuala ya ukosefu ya usalama tuwalinde watu wetu,Otherwise pitia huku Nyeri Town #RwareCentralHotel ukule Choma na mandazi."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved