logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto amekutana na bilionea Bill Gates katika Ikulu

Gates ambaye yuko nchini kwa ziara ya siku mbili aliwasili nchini Jumanne.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri16 November 2022 - 14:38

Muhtasari


  • Rais alitambua msaada unaotolewa na Bill & Melinda Gates Foundation nchini

Rais William Ruto amesema kuwa Serikali ya Kenya Kwanza itaendelea kushirikiana na washirika wote katika kufanikisha usalama wa chakula na huduma ya afya kwa wote.

Ruto alifichua hayo alipokutana na mwanzilishi wa Microsoft Bill Gates katika Ikulu ya Serikali, Jumatano.

Rais alitambua msaada unaotolewa na Bill & Melinda Gates Foundation nchini.

"Tunashukuru uungwaji mkono unaoendelea kutoa kwa Kenya katika kutimiza malengo yetu ya maendeleo, haswa katika nyanja za afya, kilimo na sekta ya ICT," Ruto alisema.

Gates ambaye yuko nchini kwa ziara ya siku mbili aliwasili nchini Jumanne.

Ametembelea Makueni na alitazamiwa kutangaza dhamira ya kuunga mkono ubunifu mpya na werevu unaolenga kuboresha afya, usalama wa chakula na usawa wa kijinsia katika nchi za Afrika.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved