logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mvulana,14,apatikana amefariki nyumbani kwao Nairobi

Mwili ulikuwa na michubuko na majeraha mgongoni, kifuani na kwenye paji la uso.

image
na

Habari23 November 2022 - 09:25

Muhtasari


  • Bidan Mburu, mwanafunzi wa Shule ya Msingi ya Zawadi jijini Nairobi alipatikana amefariki katika nyumba yao Jumanne asubuhi
  • Mwili ulikuwa na michubuko na majeraha mgongoni, kifuani na kwenye paji la uso

Sintofahamu imeshuhudiwa kuhusu kifo cha mvulana wa miaka 14 katika mtaa wa California, Nairobi.

Bidan Mburu, mwanafunzi wa Shule ya Msingi ya Zawadi jijini Nairobi alipatikana amefariki katika nyumba yao Jumanne asubuhi.

Mwili ulikuwa na michubuko na majeraha mgongoni, kifuani na kwenye paji la uso.

Familia ilisema mvulana huyo alikuwa nje ya shule kwa wiki tatu kutokana na masuala ya kinidhamu.

Polisi walisema walipigiwa simu na kufahamishwa kuhusu kupatikana kwa mwili huo kitandani.

Timu iliyotembelea eneo la tukio ilisema iliarifiwa mvulana huyo alirudi usiku wa manane Jumatatu akiwa na shati lililochanika huku akionekana kupigwa na kulala na kukutwa amefariki asubuhi.

Haijulikani alikuwa na nani na ikiwa walimpiga. Polisi walisema wanachunguza tukio hilo.

Mwili huo ulihamishwa hadi katika chumba cha kuhifadhia maiti ukisubiri uchunguzi zaidi na uchunguzi wa maiti.es

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved