logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jinsi juhudi za mwanamke za kupenyeza bangi kwa mumewe gerezani zilivyositishwa

Mwanadada huyo alikuwa ameficha bangi na sigara kwenye mkate na ndani ya suruali yake.

image
na Radio Jambo

Habari28 November 2022 - 03:43

Muhtasari


• Mwanadada anazuwiliwa kwenye kituo cha polisi cha Gilgil huku uchunguzi zaidi dhidi yake ukiendelea.

• Mwanadada huyo alijaribu kuwahonga maafisa wa polisi kwa shilingi 2,000.

Mwanamke mmoja anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Gilgil baada ya kupatikana akijaribu kupeleka bangi kwa mumewe aliyekuwa amekamatwa.

Caroline Imenza mwenye umri wa miaka 30 alifika kituoni mnamo Jumapili, Novemba 27 majira ya asubuhi na kuomba kumwona mumewe Stephen Nyabuto ambaye alikuwa anazuiliwa.

Imenza, ambaye kwa mtazamo tu hangeshukiwa kuwa na mipango mingine ya kando alikuwa amebeba mkate na kibuyu kilichojaa chai moto, ili mumewe akabadhiwe kama kiamsha kinywa chake.

Kulingana na ripoti ya DCI, afisa wa polisi aliyekuwa katika zamu wakati huo aliamua kuufungua mkate huo na kupata misokoto mitano ya bangi, sigara tano na kiberiti katikati ya mkate huo.

Bila kusita, afisa huyo alimkamata mwanadada huyo na kumfungia kwenye seli kabla ya  uchunguzi wa kina kufanyika. Mshukiwa pia alipatikana na bangi misokoto 80 mingine ya bangi  kwenye suruali yake ya ndani.

Juhudi za mshukiwa za kuwahonga maafisa hao kwa shilingi 2,000 ili kuachiliwa ziliangulia patupu. 

''Tunapopongeza hatua ya afisa wa polisi aliyekuwa kwenye zamu na wenzake, mtuhumiwa kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha Polisi huku akisubiri kufikishwa mahakamani''ripoti ya polisi ilisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved