logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Edwin Sifuna ajibu madai ya Ruto kuhusu njama ya kumuua Chebukati

Chebukati alisema uchunguzi huo utafichua fitina baada ya kura ya urais mnamo Agosti 9

image
na Radio Jambo

Habari17 January 2023 - 15:49

Muhtasari


  • Hii ni baada ya mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati, makamishna Abdi Guliye na Boya Molu kumtaka rais William Ruto kuunda tume ya uchunguzi
Mgombea wa useneta wa Nairobi Edwin Sifuna wakati wa kibali Kasarani.

Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna amewataka Wakenya wanaotoa madai ya machafuko ya Bomas kujiandaa kutoa ushahidi mbele ya tume ya uchunguzi ambayo bado haijaundwa.

Katika taarifa siku ya Jumanne, Sifuna alisema wanapaswa kuwa na uthibitisho wa madai hayo.

"Tuhuma nzito zinazotolewa kuhusiana na kile kilichotokea Bomas katika kuelekea kutangazwa kwa matokeo ya Urais," alisema.

"Ninatumai watu wanaowasilisha watafikishwa mbele ya tume ya uchunguzi ambayo bado haijaundwa na kutoa ushahidi unaounga mkono madai haya."

Hii ni baada ya mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati, makamishna Abdi Guliye na Boya Molu kumtaka rais William Ruto kuunda tume ya uchunguzi.

Chebukati alisema uchunguzi huo utafichua fitina baada ya kura ya urais mnamo Agosti 9 katika Kituo cha Kitaifa cha Kuhesabu kura katika eneo la Bomas of Kenya.

"Matokeo ya Uchunguzi yataimarisha uhuru wa Tume na kuhakikisha kwamba inadumisha hadhi inayopendekezwa na Katiba ya Kenya," Chebukati alisema.

Hafla ya kustaafu rasmi kwa watatu hao kutoka IEBC iliandaliwa jijini Nairobi na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo rais William Ruto ambaye awali amenukuliwa mara kadhaa akimtaja Chebukati kama shujaa aliyesimamamia ukweli katika uchaguzi wa Agosti mwaka jana.

Katika hotuba yake kwenye hafla hiyo, rais Ruto alisisitiza kuwa wana ufahamu kuwa kulikuwepo na njama na kumteka nyara mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati na kumuua baada ya kukataa kukubaliana na kile ambacho Ruti alisema ni kurubuni kwa matokeo ghushi ya kumtangaza mpinzani wake Raila Odinga kama rais.

“Pia tuna habari kuwa kulikuwepo na jaribio la moja kwa moja la kumteka nyara Wafula Chebukati na kumuua ili tume ya IEBC ilemazwe au kamishna mbadala achukue hatamu na kubatilisha kile ambacho wananchi walikuwa wameamua. Ulikuwa ni wakati mgumu, vitisho vilikuwa vingi, ahadi za kumezewa mate nyingi na shinikizo lilikuwa juu,” Rais Ruto alisema.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved