logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DP Gachagua akutana na MCAs wa Kericho, atangaza uongozi mpya

MCA wa Kamasian Philip Rono sasa ndiye kiongozi wa wengi, Phancy Chepkorir naibu kiongozi wa wengi,

image
na Radio Jambo

Yanayojiri19 January 2023 - 12:51

Muhtasari


  • DP Gachagua alibainisha kuwa amefanya mazungumzo na viongozi katika Bunge la Kaunti na kufikia uamuzi wa kusuluhisha ugomvi huo

Naibu Rais Rigathi Gachagua amerekebisha mgawanyiko kati ya viongozi katika Bunge la Kaunti ya Kericho kufuatia kutofautiana kuhusu uongozi wa nyumba.

Haya yanajiri kufuatia kizaazaa kilichoshuhudiwa katika Bunge la Kaunti wiki jana, ambapo video moja kwa moja iliwaonyesha baadhi ya Wabunge wa Bunge la Kaunti (MCAs) wakizozana , hali iliyosababisha Rais William Ruto kutoa onyo kali kwa viongozi hao.

Nyadhifa zilizoleta mzozo ni zile za kiongozi wa wengi, naibu kiongozi wa wengi, kinara wa walio wengi.

Kwenye kikao na wanahabari mnamo Alhamisi, DP Gachagua alibainisha kuwa amefanya mazungumzo na viongozi katika Bunge la Kaunti na kufikia uamuzi wa kusuluhisha ugomvi huo.

Akifuata ombi la Rais Ruto la kusuluhisha suala hilo, DP Gachagua alibainisha kuwa ni muhimu kusuluhisha maswala hayo kwa kuwa kaunti hiyo inashikilia nafasi ya juu katika siasa na utoaji huduma utalemazwa.

"Rais alinipa jukumu la kualika uongozi wa nchi hii kwa mkutano wa kutatua masuala yaliyosababisha mzozo huo kwa nia ya kurejesha hali ya kawaida," alisema Gachagua.

"Baada ya mashauriano, tumeona kuwa mgogoro huo unatokana na mapambano ya watu kuongoza na kutoelewana juu ya uongozi wa nyumba. Viongozi wamekubaliana kwa kauli moja kwamba tunatatua masuala yote yaliyosimama kwa amani na tunarudisha amani."

Gachagua alibainisha zaidi kuwa viongozi hao walikubaliana kufanya uchaguzi wa kuchagua viongozi wao, na kwa kauli moja kufikia uamuzi wa viongozi mahususi watakaokalia viti hivyo.

MCA wa Kamasian Philip Rono sasa ndiye kiongozi wa wengi, Phancy Chepkorir naibu kiongozi wa wengi, Aaron Rotich kinara wa wengi na Bavina Serem naibu kinara wa wengi.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved