logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mke wa mwanamume aliyezama kwenye bwawa afichua mazungumzo yao ya mwisho

Kulingana na Kiiru, hakujua kuhusu kifo cha mumewe hadi alipopokea simu kutoka kwa rafiki yake

image
na Radio Jambo

Habari19 January 2023 - 12:22

Muhtasari


  • Kiiru anadai kuwa baada ya mazungumzo yao ya hivi majuzi, alimpigia mumewe simu na hakuweza kupokea

Mke wa mwanamume aliyeangamia baada ya gari lake kutumbukia kwenye bwawa la maji huko Juja, wilaya ya Titanic kaunti ya Kiambu, hatimaye amezungumza kufuatia mkasa huo Jumatatu usiku.

Kulingana na Citizen Digital Margaret Kiiru alidai kuwa mumewe Titus Maina alikuwa mfanyabiashara aliyefanikiwa ambaye aliishi maisha kwa kuuza vifaa vya kiufundi.

"Siku ya Jumatatu asubuhi, mume wangu aliondoka kwenda kazini, na tulizungumza jioni karibu saa 7. Mara ya mwisho tulipozungumza, alisema alikuwa Juja kwa mkutano wa biashara, nilimuuliza kuhusu upendeleo wake wa chakula cha jioni, na ndivyo ilivyokuwa." Alisema.

Kiiru anadai kuwa baada ya mazungumzo yao ya hivi majuzi, alimpigia mumewe simu na hakuweza kupokea.

"Nilimpigia simu na kumtumia ujumbe lakini hakupatikana, jambo lisilo la kawaida kwake kwa sababu amekuwa akipatikana kila mara."

Kulingana na Kiiru, hakujua kuhusu kifo cha mumewe hadi alipopokea simu kutoka kwa rafiki yake mnamo Jumanne mwendo wa saa nane jioni, akimwambia aende katika kituo cha polisi cha Kimbo.

Kiiru akizungumzia mwanamke aliye kufa maji na mumewe alisema;

"Ingawa simfahamu, naamini mwanamke ambaye alikuwa na mume wangu usiku huo alikuwa rafiki, alikuwa na marafiki wengi kwa sababu ya aina ya biashara yake," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved