logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Siko tayari kumwapisha Raila tena-Miguna aweka wazi

Aidha alimshutumu Raila kwa ulaghai, akisisitiza kuwa wakati huu, Waziri Mkuu huyo wa zamani yuko peke yake.

image
na Radio Jambo

Burudani25 January 2023 - 09:02

Muhtasari


  • Aidha alimshutumu Raila kwa ulaghai, akisisitiza kuwa wakati huu, Waziri Mkuu huyo wa zamani yuko peke yake

Wakili Miguna Miguna amesema hatapatikana ili kumuapisha Raila Odinga kama 'Rais wa Wananchi' kwa mara ya pili.

Miguna pia alisema hayuko tayari kuwasaidia viongozi wa upinzani kuwarai wafuasi wao kutomtambua William Ruto kama Rais halali wa Kenya.

Aidha alimshutumu Raila kwa ulaghai, akisisitiza kuwa wakati huu, Waziri Mkuu huyo wa zamani yuko peke yake.

"Tafadhali mwambie @RailaOdinga  Mkuu @MigunaMiguna hapatikani kumwapisha kama Rais wa Wananchi, wala siko tayari kumsaidia kugomea au kumpinga Rais ALIYECHAGULIWA HALALI wa Jamhuri ya Kenya. Yule mwoga na msaliti yuko peke yake!"

Matamshi ya Miguna yanajiri siku chache baada ya  tangazo la Raila wakati wa mkutano wa Kamukunji Jumatatu kwamba Ruto aliiba kura ya urais ya Agosti 9, 2022.

"Hatutambui utawala wa Kenya Kwanza kama serikali halali na Ruto kama rais au afisa yeyote katika serikali yake," Raila alisema.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved