logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KWS yatetea upasuaji wa vasektomi kwa simba

KWS imeeleza kwamba paka huyo mkubwa atakuwa katika mazingira magumu porini.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri30 January 2023 - 11:52

Muhtasari


•Lakini KWS imeeleza kwamba paka huyo mkubwa atakuwa katika mazingira magumu porini.

Shirika la Huduma ya Pori la Kenya (KWS) wikendi lilieleza ni kwa nini simba aliyenaswa alilazimika kufanyiwa upasuaji vasektomi mwanzoni mwa wiki jana.

Awali KWS ilisema utaratibu huo ulikusudiwa kudhibiti kizazi cha simba huyo, lakini Wakenya walihoji ni kwa nini hangeweza badala yake kumuachilia porini huku kukiwa na hatari ya wanyama hao kuangamia .

Lakini KWS imeeleza kwamba paka huyo mkubwa atakuwa katika mazingira magumu porini.

“Wanyama wa porini wanapofugwa , hupoteza silika yao ya asili na wakirudishwa porini, wanakuwa hatarini.Paka hao huishia kuwa wanyama wenye matatizo wanapotafuta mawindo rahisi,” ilisema taarifa.

KWS ilisema mzozo kati ya binadamu na wanyamapori unaosababisha majeraha na mauaji ya kulipiza kisasi ni miongoni mwa tishio kuu kwa uhifadhi wa simba nchini.

Kwa sasa, idadi ya simba nchini Kenya inakadiriwa kuwa 2,589, kulingana na KWS.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved