logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Sponsors' watawapotosha-Dorcas Gachagua kwa vijana

Dorcas  alisema chaguo la mwenzi linaweza kumfanya au kumvunja mtu mdogo.

image
na Radio Jambo

Makala02 March 2023 - 14:22

Muhtasari


  • Dorcas alionya dhidi ya kitendo hicho ambacho kimeonekana kuwa ‘trend’ hasa kwenye mitandao ya kijamii
Mama Dorcas Gachagua

Kuchumbiana na wanaume wazee na wanawake wazee kutakuvunja moyo, Mke wa naibu Rais Gachagua Dorcas Gachagua amewaonya vijana.

Dorcas alionya dhidi ya kitendo hicho ambacho kimeonekana kuwa ‘trend’ hasa kwenye mitandao ya kijamii

"Sijui kama jina 'mama' au 'mubaba' linakupigia kengele, nakuomba kama mama, uwe mwangalifu," Alizungumza Dorcas.

Alizungumza alipohudhuria hafla ya mtoto wa kiume katika Chuo Kikuu cha Nairobi.

Dorcas  alisema chaguo la mwenzi linaweza kumfanya au kumvunja mtu mdogo.

"Shinikizo la mitandao ya kijamii kando na 'mubaba' na 'mumama' linaharibu wanafunzi wetu sio tu UoN bali ni jambo la kitaifa," alisema.

Wawili hao ni majina ya mitaani kuelezea mtu mzee ambaye yuko kwenye uhusiano na kijana. Dorcas aliwaonya wanafunzi wa UoN kutokana na kuzuru mtaa mmoja mjini ambao alisema una ‘shughuli za samaki.’

“Mungu atusaidie. Labda wao ni wageni kwako lakini mimi si mgeni katika jiji hili,” alisema.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved