logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mtu mmoja ajeruhiwa kwa kupigwa risasi huku maandamano yakishika kasi Nairobi

Mtu mmoja ameripotiwa kujeruhiwa na risasi katika Soko la Tai.

image
na

Makala20 March 2023 - 08:18

Muhtasari


• Kumeshuhudiwa mzozano baina ya polisi na waandananiji katika eneo la Kibra

Mtu mmoja ameripotiwa kujeruhiwa kwa kupigwa risasi huku maandamano ya muungano wa Azimio La Umoja yakiongezeka siku ya Jumatatu.

Katika video iliyoonekana, kundi la vijana wanaonekana wakiwa wamembeba majeruhi huyo. Mwanamume huyo anasemekana kupigwa risasi karibu na Soko la Toi.

Mfanyabiashara anasikika akisema kuwa mtu huyo ni fundi mitambo, si mwandamanaji. Waandamanaji wa Kibra wamejitokeza katika barabara ya Olympic wakiwa wamebeba mawe huku wakisubiri hatua ya kinara wa ODM Raila Odinga.

Wengine walibeba mawe yaliyojaa vichwani mwao walipokuwa wakienda barabarani. Maduka mengi yalifungwa katika eneo hilo. Baadhi ya wakazi walitembea kwa makundi makubwa huku wakiimba, huku wengine wakirusha mawe.

Kulikuwa na mzozo wa muda kati ya polisi na vijana huku baadhi ya vijana wakionekana wakirushia mawe magari ya polisi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved