logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi Wamuokoa mtoto wa siku nne aliyetupwa kwenye choo cha kanisa

NPS inasema mtoto huyo atachukuliwa na Kitengo chake maalum cha Ulinzi wa Mtoto.

image
na Radio Jambo

Habari19 April 2023 - 13:07

Muhtasari


  • Kwa msaada wa wananchi walibomoa shimo hilo la choo na kumchukua mtoto wa kike anayekadiriwa kuwa na umri wa siku nne na akionekana kuwa na afya njema.

Maafisa wa polisi kutoka Rioma, Kaunti ya Kisii wamemuokoa mtoto wa siku nne kutoka kwa choo cha shimo ndani ya boma la kanisa.

Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS) inasema mkaazi aliyehusika alisikia kilio cha mtoto mchanga kikitoka kwenye choo cha shimo ndani ya boma la Kanisa Katoliki la Rioma mnamo Jumanne, Aprili 18 na kuandikisha ripoti haraka katika Kituo cha Polisi cha Rioma.

"OCS na Maafisa kutoka kituo cha polisi walifika kwa haraka katika  eneo la tukio, takriban kilomita 1.4 kutoka kituoni," NPS inaongeza.

Kwa msaada wa wananchi walibomoa shimo hilo la choo na kumchukua mtoto wa kike anayekadiriwa kuwa na umri wa siku nne na akionekana kuwa na afya njema.

Alikimbizwa katika Hospitali ya Marani Level 4 na kukabidhiwa kwa Afisa Mkuu Muuguzi wa Kaunti ndogo.

NPS inasema mtoto huyo atachukuliwa na Kitengo chake maalum cha Ulinzi wa Mtoto.

"Tunampongeza mwananchi aliyetoa taarifa zilizofanikisha kuokolewa kwa mtoto kwa wakati, na tunamtakia mtoto wa kike, usalama na afya njema," mamlaka hiyo inaongeza.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved