logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mhubiri Ezekiel Odero akamatwa kwa madai shughuli kanisani mwake

Kanisa linalohusishwa naye la New Life Prayer Center Church pia limefungwa.

image
na

Burudani27 April 2023 - 07:57

Muhtasari


• Alikamatwa siku moja baada ya kuhojiwa kwa muda mrefu kwa madai kuwa kanisa lake pia linajihusisha na uchawi.

Mhubiri Ezekiel Odero wa kanisa la New Life Prayer Picha: CHARLES MGHENYI

Mwinjilisti Ezekiel Odero wa Kituo cha Maombi cha New Life Prayer Center na Kanisa amekamatwa kwa madai ya mahubiri ya itikadi kali kwa umma.

Alikamatwa siku moja baada ya kuhojiwa kwa muda mrefu kwa madai kuwa kanisa lake pia linajihusisha na uchawi.

Kamishna wa kanda ya Pwani Rhodah Onyancha alisema mhubiri huyo alikamatwa katika eneo la Mavueni, kaunti ya Kilifi.

Alisema hii ni kwa sababu kulikuwa na madai ya vifo vilivyoripotiwa kwenye kanisa lake.

Pia aliamuru kufungwa kwa Kituo cha New Life Prayer na Kanisa.

“Analetwa Mombasa kuhojiwa. Taarifa zaidi zitatolewa,” alisema.

Kwa sasa yuko Makao Makuu ya Polisi Pwani.

Mhubiri huyo alikanusha madai ya uchawi katika kanisa lake mbele ya makachero wa Kilifi siku ya Jumatano.

Polisi wanaofahamu matukio hayo walisema hatua ya kumwita Jumatano ilichochewa na ufukuaji unaoendelea wa miili kutoka shambani katika Msitu wa Shakahola.

Shamba hilo linahusishwa na mchungaji Paul Mackenzie wa Good News International Church.

Kufikia sasa zaidi ya miili 95 imefukuliwa kutoka kwenye makaburi katika msitu huo, maafisa walisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved