logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Huzuni! Familia yawapoteza watoto 3 katika ajali ya barabarani Kiambu

Hata hivyo, eneo la tukio lilikuwa na lori lililokuwa na skrini iliyopasuka,

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 May 2023 - 10:14

Muhtasari


  • Mama huyo alipokuwa akisimulia mkasa huo mchungu, alieleza kwamba wanne hao walimwambia walikuwa sawa mara ya mwisho alipozungumza nao.
Ajali

Familia moja iliyoko Kiambu iko katika majonzi baada ya watoto wao wanne kuhusika katika ajali mbaya ya barabarani.

Mama wa watoto hao alieleza kuwa watatu kati yao walifariki dunia wakiwa ICU. Mmoja wao alinusurika kwenye ajali hiyo.

"Walikuwa wameenda kumchukua dada yao kisha wanarudi. Nisingejua wamejikutaje hapa kwenye ajali hii," alisema.

Gazetti la The Star halikuweza kufichua jinsi ajali hiyo ilivyotokea wakati wa kuchapisha habari hii.

Hata hivyo, eneo la tukio lilikuwa na lori lililokuwa na skrini iliyopasuka, pikipiki na gari jingine likiwa na bumper iliyovunjika.

Mama huyo alipokuwa akisimulia mkasa huo mchungu, alieleza kwamba wanne hao walimwambia walikuwa sawa mara ya mwisho alipozungumza nao.

"Mara ya mwisho nilizungumza nao mida ya saa 9.30 waliniambia wako sawa. George aliondoka saa 9 kwenda kumchukua dada yake sikudhani hatarudi. Sijui waliendaje wote na alihusika," alisema.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved