logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume akamatwa kwa kumiliki kichwa na sehemu za siri za kiume

Uchunguzi ulikuwa ukiendelea ili kuwakamata wanaodaiwa kuwa wapangaji na wanunuzi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri11 May 2023 - 11:54

Muhtasari


  • Watoto waligundua sehemu za miili hiyo kwenye mfuko wa plastiki katika wilaya ya Nhamatanda na kutoa taarifa kwa mamlaka
Mwanamume akiwa ametiwa pingu ndani ya seli.

Mwanaume mmoja amekamatwa katika jimbo la kati la Sofala nchini Msumbiji kwa kumiliki kichwa na sehemu za siri za mwanaume, polisi wamesema.

Watoto waligundua sehemu za miili hiyo kwenye mfuko wa plastiki katika wilaya ya Nhamatanda na kutoa taarifa kwa mamlaka, alisema Dércio Chacate, msemaji wa kamandi ya polisi ya Sofala.

Uchunguzi ulipelekea kukamatwa kwa mtu huyo ambaye alikiri kumuua mtu kisha kumkata kichwa na sehemu zake za siri ili aweze kuziuza, alisema.

Mshukiwa alikiri kuua na kukata vichwa vya watu wengine watatu, Bw Chacate alisema.

Uchunguzi ulikuwa ukiendelea ili kuwakamata wanaodaiwa kuwa wapangaji na wanunuzi.

Viungo vya mwili hutumiwa na baadhi ya wanaoitwa madaktari wa jadi kutengeneza dawa, ambazo kwa uwongo wanadai zinaweza kutibu magonjwa, kuondoa dalili mbaya na kuboresha maisha ya watu.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved