logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chama cha wamiliki wa matatu nchini kuongeza nauli kuendana na bei mpya ya mafuta

Jumapili, Mei 14, EPRA iliongeza bei za Super Petrol, Dizeli na Mafuta ya Taa kwa Ksh3.40 kwa lita,

image
na Radio Jambo

Burudani15 May 2023 - 12:37

Muhtasari


  • Mwenyekiti wa Chama cha wamiliki wa matatu (daladala) nchini , Samuel Kimutai akizungumza amesema kuwa serikali inapaswa kurejesha ruzuku.

Chama cha wamiliki wa matatu nchini Kenya wamesema hawana budi bali kuwatwisha abiria mzigo huo wa bei ya mafuta kwa kuongeza nauli kuendana na bei mpya ya mafuta ya petroli na dizeli.

Mwenyekiti wa Chama cha wamiliki wa matatu (daladala) nchini , Samuel Kimutai akizungumza amesema kuwa serikali inapaswa kurejesha ruzuku.

"Serikali inafaa kufikiria kurejesha ruzuku hizo kwani hii inaathiri Wakenya wanaoenda kwenye shughuli zao za kila siku ili kukuza uchumi," alisema Kimutai.

Jumapili, Mei 14, EPRA iliongeza bei za Super Petrol, Dizeli na Mafuta ya Taa kwa Ksh3.40 kwa lita, Ksh6.40 kwa lita na Ksh15.19 kwa lita mtawalia.

Ongezeko hili linamaanisha bei ya petroli imeongezeka hadi shilingi 182.70, ile ya dizeli ikipanda hadi 168.40 na mafuta taa yatauzwa kwa shilingi 161.13 jijini Nairobi.

“Kwa mujibu wa Kifungu cha 101(y) cha Sheria ya Petroli ya 2019 na Notisi ya Kisheria Na.192 ya 2022,EPRA imepania kubadilisha bei za juu zaidi za rejareja na za jumla za bidhaa za petroli ambazo zitaanza kutumika kuanzia tarehe 15Mei hadi tarehe 14 Juni 2023.” Taarifa hio ilisoma.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved