logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu watatu wamefariki baada ya tuk-tuk kugongana na lori Kilifi

Watu watatu walifariki Jumatatu baada ya tuk-tuk kugongana na lori eneo la Kwakazuri mjini Kilifi.

image
na

Yanayojiri16 May 2023 - 10:59

Muhtasari


• Watu wengine watatu katika tuk-tuk wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya kaunti ya Kilifi. Wawili wako katika hali mbaya.

• Fredrick Kadzo, mkazi, alipoteza wapendwa wawili katika ajali hiyo.

Watu watatu walifariki Jumatatu usiku baada ya tuk-tuk waliyokuwa wakisafiria kugongana na lori eneo la Kwakazuri kando ya barabara kuu ya Kilifi-Malindi.

Watu wengine watatu katika tuk-tuk wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya kaunti ya Kilifi. Wawili wako katika hali mbaya.

Kamanda wa polisi wa gatuzi Ndogo ya Kilifi Kaskazini Kenneth Maina alisema watu wawili akiwemo dereva wa tuk-tuk walifariki papo hapo huku mtu wa tatu akiaga dunia alipokuwa akipokea matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Kilifi.

Wawili kati ya waliofariki ni watu wa ukoo.

“Tuk-tuk ilikuwa imejaa kupita kiasi na ilikuwa ikielekea Tezo kutoka Kilifi. Ilikuwa na watu sita akiwemo dereva. Dereva wa tuk-tuk alikuwa akipita trela na kugongana uso kwa uso na lori hilo,” alisema.

Maina Alisema ajali hiyo ilitokea majira ya saa nne usiku.

Fredrick Kadzo, mkazi, alipoteza wapendwa wawili katika ajali hiyo.

Kulingana na Kadzo, jamaa zake Edgar Kadzo na Kilian Chiro wote ni madereva wa tuk-tuk.

“Edgar ni kaka yangu na Chiro ni mpwa wangu. Wote ni madereva wa tuk-tuk na walikuwa wakielekea nyumbani ajali ilipotokea," alisema.

"Walikuwa wamechukua abiria huko Kilifi na walitakiwa kuwafikisha Tezo na kisha kuelekea nyumbani. Nilizungumza nao jioni na saa 10:30 jioni nikapokea taarifa za kufariki kwao. Ni uchungu mkubwa kupoteza wapendwa wangu kwa wakati mmoja."

Miili hiyo ilihamishwa hadi katika makao ya maiti ya hospitali ya kaunti ya Kilifi ikisubiri uchunguzi wa maiti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved