logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Dhehebu la Shakahola: Serikali kupanua msako wa miili hadi mbuga ya Tsavo

Miili zaidi ya 230, tayari imefukuliwa na idadi ya miili zaidi inatarajiwa kufukuliwa

image
na Radio Jambo

Habari22 May 2023 - 03:53

Muhtasari


•Kindiki amesema kuwa serikali itatumia droni kusaidia juhudi za wachunguzi wanaofanya msako wa miili ardhini.

Msako wa wa manusura na miili ya watu waliokufa kutokana na mfungo katika dhehebu ‘tata’ la msitu wa Shakahola , Kilifi nchini Kenya utapanuliwa hadi katika Mbuga ya Wanyama ya taifa ya Tsavo East, Waziri wa mambo ya ndani wa Kenya Kithure Kindiki , amenukuliwa na vyombo vya habari Jumamosi akisema.

Amesema kuwa serikali itatumia droni kusaidia juhudi za wachunguzi wanaofanya msako wa miili ardhini huku mchakato wa kufukua miili katika makaburi ya pamoja uliwa umesimamishwa ili kuruhusu uchunguzi wa maiti ufanyike .

"Msako wa manusura na miilindani yam situ wa Shakahola na katikaChakama Ranch kwa ujumla utaendelea bila kuvurugwa na utapanuliwa hadi ndani ya mbuga ya Wanyama ya taifa-Tsavo East National Park katika siku zijazo kwa msako wa ardhini na wa anga kwa kutumia droni," alisema wazir Kindiki katika taarifa yake.

Ijumaa watu zaidi waliokolewa katika msitu wa Shakahola, na hivyo kupelekea idadi ya watu waliookolewa katika tukio ambapo mchungaji Paul Mackenzie Nthenge wa kanisa la Good News International aliripotiwa kuwaagiza wafuasi wake kufunga hadi kufa ili ‘’kukutana na Yesu’’ kufikia 90.

Miili zaidi ya 230, tayari imefukuliwa na idadi ya miili zaidi inatarajiwa kufukuliwa, kulingana na maafisa.

Shughuli ua kufukua miili ilisitishwa Alhamisi ili kutoa fursa ya uchunguzi wa miili , na inatarajiwa kuanza tena Jumatano wiki ijayo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved