Serikali kujenga nyumba 20,000 za bei nafuu Bungoma-Ruto

Ili kurahisisha biashara, Ruto pia aliahidi kujenga na kukamilisha ujenzi wa barabara za Bungoma.

Muhtasari
  • Mkuu wa nchi alisema mradi huo pia utatoa fursa za ajira kwa takriban vijana 40,000 huko Bungoma.
Ruto
Ruto
Image: Facebook

Rais William Ruto amesema kuwa serikali imejitolea kujenga nyumba 20,000 katika Kaunti ya Bungoma kama sehemu ya mpango wa nyumba za bei nafuu.

Mkuu wa nchi alisema mradi huo pia utatoa fursa za ajira kwa takriban vijana 40,000 huko Bungoma.

"Tunaposhughulika na mpango wa nyumba za bei nafuu, tunataka kujitolea kujenga nyumba 20,000 za bei nafuu huko Bungoma, nyumba hizo 20,000 zitahitaji takriban vijana 30,000 hadi 40,000 kufanya kazi katika mradi huo," Ruto alisema.

Ruto zaidi aliahidi wakazi kwamba kila kata itakuwa na vituo vya ICT ili kuboresha ufikiaji wa mtandao na hivyo kutoa kazi za kidijitali.

Aidha aliapa kuondoa makundi yanayowahujumu wakulima wa ndani kwa njia ya ulaghai.

Pia aligusia suala la miundombinu ya soko alipofafanua kuwa serikali itajenga masoko 10 ya ziada mjini Bungoma ili kurahisisha biashara.

Ili kurahisisha biashara, Ruto pia aliahidi kujenga na kukamilisha ujenzi wa barabara za Bungoma.