logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tazama maeneo ambayo yatakuwa bila stima Jumapili, Novemba 26- KPLC

Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Kajiado, Trans Nzoia, Machakos na Uasin Gishu.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri26 November 2023 - 05:48

Muhtasari


•Jumamosi jioni, KPLC ilitoa ilani kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa siku ya Jumapili, Novemba 26.

•Katika kaunti ya Kajiado, umeme utatizwa katika sehemu za maeneo ya Ngong, Kibiko na Ngong Kerarapon kati ya saa tatu

Jumamosi jioni, Kampuni ya Kusambaza Umeme Nchini (KPLC)  ilitoa ilani kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa siku ya Jumapili, Novemba 26.

Katika taarifa yake, kampuni hiyo ilitangaza kuwa baadhi ya maeneo katika kaunti nne za Kenya yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Kajiado, Trans Nzoia, Machakos na Uasin Gishu.

Katika kaunti ya Kajiado, umeme utatizwa katika sehemu za maeneo ya Ngong, Kibiko na Ngong Kerarapon kati ya saa tatu. Maeneo hayo yameratibiwa kukosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za barabara ya Kangundo katika kaunti ya Machakos pia zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni. Sehemu zitakazoathirika ni pamoja na Kangundo Rd, Joska, Malaa, Koma Hill, Tala, Kangundo, Kikomba, Kyevaluki, Isooni, Kivaani na maeneo ya karibu.

Katika kaunti ya Trans Nzoia, baadhi ya sehemu za maeneo ya Natwana na Makunga zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri.

Maeneo ya Diesel Power na Action katika kaunti ya Uasin Gishu pia zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa nne asubuhi na saa tisa alasiri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved