Raila Odinga a'dedicate siku ya kuzaliwa kwa Watoto huko Palestina

"Kinachotokea Gaza ni mauaji ya halaiki. Watoto ni maua ya taifa na ikiwa hakuna watoto basi nchi haiwezi kustawi," alisema.

Muhtasari

• "Kinachotokea Gaza ni mauaji ya halaiki. Watoto ni maua ya taifa na ikiwa hakuna watoto basi nchi haiwezi kustawi," alisema.


• Kiongozi huyo wa upinzani alimtaka Rais William Ruto kulaani kuendelea kwa mauaji ya watoto huko Gaza.

Raila Odinga akisherehekea siku yake ya kuzaliwa na watoto mayatima.
Raila Odinga akisherehekea siku yake ya kuzaliwa na watoto mayatima.
Image: ELIAS YAA//THE-STAR

Kinara wa ODM Raila Odinga amesherehekea siku yake ya kuzaliwa ya 79 na watoto kutoka nyumba nane za watoto huko Malindi.

Maadhimisho hayo yalifanyika katika kituo cha watoto yatima cha Malindi kilichopo Malindi mjini.

Raila aliadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa ukombozi wa watoto na watu wa Palestina.

Kiongozi huyo wa ODM alisikitishwa na kuzorota kwa ustawi wa watoto katika Ukanda wa Gaza kufuatia kuendelea kwa mashambulizi ya mabomu.

"Kinachotokea Gaza ni mauaji ya halaiki. Watoto ni maua ya taifa na ikiwa hakuna watoto basi nchi haiwezi kustawi," alisema.

Kiongozi huyo wa upinzani alimtaka Rais William Ruto kulaani kuendelea kwa mauaji ya watoto huko Gaza.

"Nataka kumwambia William Ruto kwamba anapaswa kulaani mashambulizi yanayoendelea. Huwezi kuendelea kuua watoto hata kama umeudhika. Ninaihurumia Israel kwa kilichotokea lakini Israel isiwafanye Wapalestina kuwa wakimbizi katika nchi yao. Kinachoendelea Gaza ni sawa na kile Hitler alifanya," aliongeza.

Mkewe Raila Odinga Ida Odinga alisema watoto wote ni wa Mungu.

Alimshukuru Raila kwa kujumuika na watoto hao kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Watoto watano pia walikuwa wakisherehekea siku yao ya kuzaliwa na Raila.

Raila alitoa chakula cha mwezi mmoja kwa kila nyumba ya watoto wanane.

Pia alitoa Sh500,000.

Viongozi wengine waliopamba hafla hiyo ni Gavana wa Mombasa Abdulswamad Nassir, naibu gavana wa Kilifi Flora Chibule, Seneta wa Kilifi Stewart Madzayo, wabunge Ken Chonga (Kilifi Kusini), Amina Mnyazi (Malindi), Harry Kombe (Magarini) Mishi Mboko (Likoni), Rashid Bedzimba. (Kisauni) miongoni mwa viongozi wengine.