logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme Jumanne

Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Machakos, Kajiado, Makueni, Uasin Gishu, Kilifi na Mombasa.

image
na Radio Jambo

Burudani06 February 2024 - 05:32

Muhtasari


•KPLC ilisema baadhi ya maeneo ya kaunti saba za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

•Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Machakos, Kajiado, Makueni, Uasin Gishu, Kilifi na Mombasa.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumanne, Februari 6.

Katika taarifa ya siku ya Jumatatu jioni, kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti saba za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni. Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Nairobi, Machakos, Kajiado, Makueni, Uasin Gishu, Kilifi na Mombasa.

Baadhi ya sehemu za barabara ya Outering na eneo la Donholm Phase 8 katika kaunti ya Nairobi zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Machakos, sehemu kadhaa za maeneo ya Matuu, Sofia, Kyumbi, na Kitui Road  zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tisa asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Wakati huo huo, baadhi ya sehemu za maeneo ya Emali Ukia Roa na Kaumoni katika kaunti ya Makueni pia zitakosa umeme.

Sehemu kadhaa za maeneo ya Kajiado, Kisaju na Isinya katika kaunti ya Kajiado zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Uasin Gishu, sehemu za maeneo ya Burnt Forest na Kondoo zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Kasufini na Mkoamoto katika kaunti ya Uasin Gishu zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tisa asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu kadhaa za eneo la Utange katika kaunti ya Mombasa zitakosa umeme kati ya saa tatu na saa kumi na moja jioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved