logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tazama maeneo ambayo yataathirika na kukatizwa kwa umeme Alhamisi

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Nairobi, Machakos, Busia,Kajiado, Meru, Kilifi, Mombasa na Tana River.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 February 2024 - 05:25

Muhtasari


•Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Nairobi, Machakos, Busia,Kajiado, Meru, Kilifi, Mombasa na Tana River.

•Sehemu kadhaa za maeneo ya Westlands na Upperhill yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Februari 8.

Katika taarifa ya Jumanne jioni, kampuni hiyo ilitangaza kuwa baadhi ya maeneo ya kaunti saba za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni. Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Nairobi, Machakos, Busia,Kajiado, Meru, Kilifi, Mombasa na Tana River.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu kadhaa za maeneo ya Westlands na Upperhill yatakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Tala, Kangundo, na Machakos Eastleigh katika kaunti ya Machakos zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu kadhaa za maeneo ya Mungatsi na Kwangamor katika kaunti ya Busia zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Kajiado, sehemu kadhaa za eneo la Korompoi zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni

Sehemu kadhaa za maeneo ua Urru na Miathene katika kaunti ya Meru pia zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Wakati huohuo, baadhi ya sehemu za eneo la Watamu katika kaunti ya Kilifi zitaathirika na kukatizwa kwa umeme.

Katika kaunti ya Mombasa, sehemu za eneo la Miritini zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Hola na Bura katika kaunti ya Tana River pia zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved