logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KPLC yatangaza maeneo ambako stima zitapotea Alhamisi

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na  Nairobi, Samburu, Nyeri, Murang'a na Kilifi.

image
na Radio Jambo

Habari02 May 2024 - 04:23

Muhtasari


•KPLC ilisema baadhi ya maeneo ya kaunti 5 za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Mei 2.

Katika taarifa ya siku ya Jumatano jioni, kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti tano za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na  Nairobi, Samburu, Nyeri, Murang'a na Kilifi.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu kadhaa za mtaa wa Peponi zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Mji mzima wa Maralal na eneo la Posta katika kaunti ya Samburu kutakuwa bila umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti za Murang'a na Nyeri, baadhi ya sehemu za maeneo ya Kiriani na Kamune zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Shamba la Kilifi katika kaunti ya Kilifi pia litaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved