logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shirika la Reli la Kenya (KRC) Larejesha Huduma ya Treni kwa Wasafiri

Huduma katika Kijiji cha Embakasi, Lukenya, SGR Link na njia za Syokimau kurejelewa leo.

image
na

Yanayojiri07 May 2024 - 06:07

Muhtasari


•Njia za Limuru na Ruiru zitaendelea kusimamishwa kutokana na ukarabati.

• Huduma katika Kijiji cha Embakasi, Lukenya, SGR Link na njia za Syokimau zitarejelewa  kuanzia kuanzia leo Jumanne

Mamlaka ya Reli ya Kenya

Shirika la Reli la Kenya (KRC) limetangaza kurejeshwa kwa baadhi ya huduma za treni ya abiria baada ya kusimamishwa kutokana na mvua kubwa inayonyesha.

KRC mnamo Aprili 24 ilisimamisha treni ya abiria ambayo husafirisha wasafiri kwenda na kutoka katikati mwa jiji la Nairobi kila siku katika njia tano; Embakasi, SGR Link na Syokimau, Limuru, Lukenya na Ruiru

Siku ya Jumatatu, Shirika la Reli la Kenya lilisema katika taarifa kwa umma kuwa litarejelea huduma katika Kijiji cha Embakasi, Lukenya, SGR Link na njia za Syokimau kuanzia leo Jumanne.

Hata hivyo, njia za Limuru na Ruiru zitaendelea kusimamishwa kutokana na ukarabati unaoendelea kwenye njia za reli, ilisema.

"Pia tungependa kushauri umma kwamba huduma za treni za abiria zinaweza kubadilika, kulingana na hali ya hewa na masuala mengine ya usalama. Tunashukuru kwa subira  tunapojitahidi kurejesha hali ya kawaida,” ilisema taarifa ya umma kutoka kwa usimamizi wa KRC.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved